Tanzania emblem
The United Republic of Tanzania

Prime Minister's Office

Labour, Youth, Employment and Persons with Disability

News

WAZIRI MHAGAMA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA VIONGOZI WA ATE NA TUCTA



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na viongozi wa Chama cha Waajiri (ATE) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) walipokutana kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya Wafanyakazi na Waajiri, Novemba 2, 2019 Jijini Dodoma.

Sehemu ya viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipokutana nao Bungeni, Jijini Dodoma. Kushoto ni Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe akifafanua jambo wakati wa kikao hicho cha Utatu kilichowakutanisha kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya Wafanyakazi na Waajiri.

Baadhi ya wajumbe kutoka Chama cha Waajiri (ATE) na Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia majadiliano wakati wa mkutano huo uliofanyika Jijini Dodoma.

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya akieleza jambo wakati wa mkutano huo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akipitia taarifa wakati wa mkutano na viongozi wa Chama cha Waajiri (ATE) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) walipokutana kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya Wafanyakazi na Waajiri, Jijini Dodoma.

Mkuu wa Huduma za Kisheria kutoka Chama cha Waajiri (ATE) Bi. Suzan Ndomba akichangia mada wakati wa mkutano huo uliofanyika Jijini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe.