News
Waziri Sangu ashiriki mazishi ya Asha Golaza
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (Mb), ameshiriki katika ibada ya mazishi ya marehemu Asha Golaza yaliyofanyika leo 17 Desemba 2025, Nkuhungu Jijini Dodoma.
Aidha, Marehemu Asha alikuwa Mtumishi wa Ofisi hiyo, akihudumu nafasi ya Mpokezi Mkuu.
Mazishi hayo yamehudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Mary Maganga, Wakurugenzi na Watumishi, ambapo waliungana na familia ya Golaza kuhifadhi mwili wa marehemu.
