Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akipokea tuzo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda kwa kutambua mchango wake mkubwa katika usimamizi wa masuala ya usalama na afya mahali pa kazi pamoja kutambua juhudi zake katika uboreshaji wa mazingira ya kazi nchini. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mary Maganga.